mwanazuoni

MIKOA YA TANZANIA BARA

1
MIKOA YA TANZANIA BARA.
Na. Mkoa
1 Arusha
2 Dar Es Salaam
3 Dodoma
4 Iringa
5 Kagera
6 Kigoma
7 Kilimanjaro
8 Lindi
9 Manyara
10 Mara
11 Mbeya
12 Morogoro
13 Mtwara
14 Mwanza
15 Pwani
16 Rukwa
17 Ruvuma
18 Shinyanga
19 Singida
20 Tabora
21 Tanga
MIKOA MIPYA ITAKAYOANZISHWA
(i) Mkoa wa Njombe ambao unatokana na kumega na kuunganisha
Wilaya za Njombe, Ludewa na Makete kutoka Mkoa wa Iringa.
Mkoa huu utakuwa na Wilaya mpya ya Wanging’ombe ambayo
inatokana na kugawanywa kwa Wilaya ya Njombe.
(ii) Mkoa wa Geita ambao unatokana na kumega na kuunganisha
Wilaya za Geita kutoka Mkoa wa Mwanza, Bukombe kutoka Mkoa
wa Shinyanga na Chato kutoka Mkoa wa Kagera. Mkoa huu
utakuwa na Wilaya mpya ya Nyang’hwale ambayo inatokana na
kugawanywa kwa Wilaya ya Geita.
(iii) Mkoa wa Simiyu ambao unatokana na kumega na kuunganisha
Wilaya za Bariadi kutoka Mkoa wa Shinyanga, Maswa kutoka Mkoa
wa Shinyanga, Meatu kutoka Mkoa wa Shinyanga na Wilaya mpya
ya Busega kutoka Mkoa wa Mwanza. Mkoa huu utakuwa na Wilaya
nyingine mpya ya Itilima ambayo inatokana na kugawanywa kwa
Wilaya ya Bariadi.
2
(iv) Mkoa wa Katavi ambao unatokana na kumega na kuunganisha
Wilaya za Mpanda kutoka Mkoa wa Rukwa pamoja na Wilaya
mpya ya Mlele ambayo inatokana na kugawanywa kwa Wilaya ya
Mpanda.
MADHUMUNI YA KUANZISHWA MIKOA MIPYA
Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inaelekeza kuwa, kwa ajili ya
utekelezaji bora wa shughuli za Serikali, Mheshimiwa Rais anaweza kuigawa
Nchi katika Mikoa au Wilaya. Hivyo, madhumuni ya kuanzishwa kwa Mikoa hiyo
ni kuboresha utendaji wa Serikali Kuu kwa kupunguza ukubwa wa maeneo ya
Mikoa mama ili Wananchi wapate huduma za kiutawala ngazi ya Mikoa kwa
karibu.
Jumla ya Mikoa ya Tanzania Bara itakuwa 25 ambayo ni Arusha, Dar Es
Salaam, Dodoma, Iringa, Kagera, Kigoma, Kilimanjaro, Lindi, Manyara, Mara,
Mbeya, Morogoro, Mtwara, Mwanza, Pwani, Rukwa, Ruvuma, Shinyanga,
Singida, Tabora, Tanga, Njombe, Geita, Simiyu na Katavi
Share on Google Plus

. Mtani

Mshana is Tanzanian blogger who writes different news without bias, He provides social, political and sports as well as Entertainment news happening in all parts around the World."STAY ME ALL THE TIME FOR INSTANT UPDATES.."
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment