mwanazuoni

CCM YAMTAJA MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA CHAMBANI






Katibu wa Kamati Maalumu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM Zanzibar, Waride Bakari Jabu alisema Kamati Maalumu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM Zanzibar ilikutana mwishoni mwa wiki na ilipendekeza majina mawili likiwamo hilo la Mattar na kuwasilisha kwa Kamati Kuu ya CCM.

Kamati kuu ya halmashahuri kuu ya Taifa ya chama cha mapinduzi  kimeteua na kupitisha jina la  Mattar Saharan Said kuwa mgombea ubunge wa jimbo la Chambani, wilaya ya mkoa, mkoa wa kusini Pemba.

 Uchaguzi wa jimbo hilo unafanyika kutokana na kifo cha aliyekuwa mbunge, Salim Hemed Khamis (CUF) aliyefariki Machi 28 mwaka huu jijini Dar es Salaam wakati akihudhuria moja ya vikao vya Kamati za Bunge.



Katibu wa Kamati Maalumu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM Zanzibar, Waride Bakari Jabu alisema Kamati Maalumu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM Zanzibar ilikutana mwishoni mwa wiki na ilipendekeza majina mawili likiwamo hilo la Mattar na kuwasilisha kwa Kamati Kuu ya CCM.
Kamati hiyo ilipitisha uteuzi huo katika kikao chake cha siku moja kilichofanyika mjini Dodoma jana chini ya Mwenyekiti wake, Rais Jakaya Kikwete.
Katika kikao hicho, pia imemteua Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Balozi Seif Idd kuzindua kampeni hizo,
Mei 18 mwaka huu wakati naye Mwenyekiti mstaafu wa CCM na Rais Mstaafu wa Awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi atafunga kampeni hizo kabla ya uchaguzi Juni 6.


CHANZO: GAZETI LA MWANANCHI 16/05/2013



Share on Google Plus

. Mtani

Mshana is Tanzanian blogger who writes different news without bias, He provides social, political and sports as well as Entertainment news happening in all parts around the World."STAY ME ALL THE TIME FOR INSTANT UPDATES.."
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment