mwanazuoni

MBUNGE JOSHUA NASSARI AMKACHA MHE: HALIMA MDEE


Mbunge Arumeru Mashariki (Chadema), Joshua Samwel Nassari amefunga ndoa na Anande Nko kwenye Kanisa la Pentekoste lililopo Kilinga, Arumeru jijini Arusha ikifuatiwa na sherehe kubwa iliyofanyika katika Viwanja vya Usa-River Academy jirani na Hoteli ya Ngurdoto.

Sherehe hiyo ilianza mishale ya saa 7:00 mchana siku ya leo ambapo watu wote walialikwa wakiwemo ndugu, marafiki, jamaa na wananchi wote wa Arumeru Mashariki ambao wamepiga ‘mpunga’ wa kutosha na vinywaji hadi kila mtu akaondoka akisema ‘Nassari ameacha historia’.



Tanbih: Mbunge huyu alisema kuwa atamuoa Halima Mdee wakati wanafanya kampeni katika jimbo la Arumeru hii ni ndio sababu ya mwandishi kusema kuwa Mbunge huyu amemkacha Mhe: Halima James Mdee.
Share on Google Plus

. Mtani

Mshana is Tanzanian blogger who writes different news without bias, He provides social, political and sports as well as Entertainment news happening in all parts around the World."STAY ME ALL THE TIME FOR INSTANT UPDATES.."
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment