mwanazuoni

VIONGOZI BORA NI ZAO LA SIASA SAFI




Ili tuendelee tunahitaji vitu vikuu vine; Watu, Ardhi, Siasa safi na Uongozi bora (Azimio la Arusha 1967). Siasa safi ni kichocheo cha maendeleo. Ni utaratibu ambao watu katika nchi hujadili changamoto zinazowakabili na kupendekeza namna ya kuzitatua kwa nguvu ya hoja huku wakisisitiza umuhimu wa upendo, Amani na ustawi wa pamoja. Ni utaratibu ambao wagombea wa viti mbalimbali watashindanishwa kwa sifa, uwezo, uzoefu, hekima, busara na maalifa waliyonayo. Ni utaratibu mzuri unaowezesha kupata viongozi bila kueneza chuki, hila, majungu, udini, ukabila wala fitina miongoni mwa jamii. Ndio njia pekee ya kuliwezesha Tafa kupata viongozi bora katika hali ya Amani na mshikamano wa Kitaifa. Siasa chafu ni ile ambayo vyama vya siasa hudiliki kuandaa mikakati ya kuwagombanisha wananchi ili viweze kupata fulsa ya kutawala. Vipo tayari kuandaa mikakati ya kupoteza uhai wa baadhi ya wananchi ili viweze kuchaguliwa kushika dola. Ni Siasa za makundi, za kirasimu na kutumia pesa. Siasa ambazo Vyama vya siasa vinatafuta ushindi kwa gharama zozote pasipokuzungatia demokrasia huru na makini. Siasa chafu zimefanya watu waone ya kwamba siasa ni uwanja wa fujo na sio mfumo wa kuwawezesha kupata viongozi bora kwa njia ya Amani. Mchakato wa uchaguzi ndani na nje ya vyama shindani na katika taifa zima umetoa mwanya kwa wanasiasa kutumia mbinu zote wanazozijua ili kujipatia ushindi katika mfumo a vyama vingi vya siasa. Ushindani wa kisiasa uliopo umebaini hisia za kidini, ukabila, matumizi ya mabavu, ukanda, utofauti wa rika (vijana na wazee) na vita vya kisiasa vya wenyewe kwa wenyewe miongoni mwa wanachama wa chama husika na wananchi kwa ujumla. Taratibu za kampeni na uchaguzi zimekuwa ni za kuhujumiana wenyewe kwa wenyewe na pia kuhujumu demokrasia. Wagombea wanapandikiza chuki na kuwagawa wananchi ndani ya vyama na nje ya vyama ili kupitia mgawanyiko huo wapate mwanya wa kutawala. Wagombea wanadiliki kununua wapiga kura na hata kuandaa mkakati maalumu wa baadhi ya watu kupiga kura zaidi ya mara moja. Utaratibu wa namna hii hauwezi kujenga Taifa imara, siasa safi haipaswi kutoa mwanya kwa wagombea au vyama vya siasa kutumia mbinu hata zile zinazohatarisha uhai wa wananchi na Taifa..

  • Je Taifa letu linaendesha siasa safi?
  • Je vyama vyetu vya siasa vinaendesha siasa safi?
  • Je hatuoni sababu ya kuja na azimio lenye lengo la kujadili kwa kina maana na namna ya utekelezaji wa siasa safi, mapungufu ya demokrasia ya sasa na maana halisi ya demokrasia?

Raisi wa Marekani Abraham Licon aliwahi kusema ya kwamba’Demokrasia ni Serikali inayoundwa na kuongozwa na watu kwa ajili ya watu’ Lakini Serikali nyingi leo hususani katika Bara letu la Afrika zinaundwa na watu lakini haziwanufaishi watu isipokuwa tabaka tawala. Tabaka tawala linaishi maisha mazuri, ya kupendeza na kutamanika lakini tabaka la wapiga kura. tabaka la watawaliwa linaendelea kuwa masikini siku baada ya siku.Utekelezaji wa demokrasia ni tofauti kabisa na demokrasia yenyewe. Hakuna mtu anaehitaji demokrasia ambayo sauti ya wanyonge haisikilizwi na wala ikisikilizwa haithaminiiwi. Demokrasia halisi hailuhusu kuwepo kwa matabaka kati ya wenye nacho na wasionacho. Demokrasia halisi inaamini ya kwamba binadamu wote ni sawa hivyo wanastahli thamani inayolingana. Jamani kama utekelezaji wa demokrasia ni tofauti kabisa na maana halisi ya demokrasia hakuna sababu za kuendelea na utekelezaji wa demokrasia usiokidhi demokrasia yenyewe. Utekelezaji wa demokrasia unaokizana na maana halisi ya demokrasia unatokana na viongozi dhaifu waliopatikana kwa siasa chafu.

Tanzania ipo katika kipindi ambacho uongozi umeonekana hauna maana, haufai kutokana na kushindwa kutatua changamoto za watu kwa wakati. Watu wanaona ni bora waishi pasipo na viongozi kutokana na umuhimu wa viongozi kutokuonekana.Yote haya yamesababishwa na siasa chafu zinazotumika kuwaweka viongozi madarakani.

Nitumie fulsa hii kutoa wito kwa Watanzania wenzangu; kuangalia namna ya kuishinikiza Serikali na Bunge kutunga sharia na utaratibu utakaowezesha uendeshaji wa Siasa safi ili tuweze kupata viongozi bora. Kiandaliwe kitabu kinachoelezea namna ya kutekeleza siasa safi katika nchi yetu


Tegemeo Sambili 0717250797


 
Share on Google Plus

. Mtani

Mshana is Tanzanian blogger who writes different news without bias, He provides social, political and sports as well as Entertainment news happening in all parts around the World."STAY ME ALL THE TIME FOR INSTANT UPDATES.."
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment