mwanazuoni

RUFAA YA KUPINGA KUACHIWA ZOMBE NA WENZAKE IMESIKILIZWA LEO

Mahakama ya Rufaa imesikiliza rufaa ya kupinga kuachiwa huru kwa aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi wa Mkoa wa Dar es salaam ‘RCO’ Kamishna Msaidizi wa Polisi ‘ACPAbdallah Zombe na askari wenzake watatu waliokuwa wanakabiliwa na mashitaka ya mauaji.
Rufaa hiyo imesikilizwa mbele ya jopo la majaji watatu ambapo wamesikiliza pande zote mbili wa mashitaka na utetezi na itatoa maamuzi baada ya majaji kupitia kesi hiyo.
Mkurugenzi wa Mashitaka ‘DPP’ alikata rufaa mwaka 2013 akipinga hukumu ya Mahakama Kuu Kanda ya Dar es salaam iliyowaachia huru Zombe na wenzake baada ya kuwaona hawana hatia katika kesi ya mauaji ya watu wanne iliyokuwa inawakabili.
 Aliyewahi kuwa mkuu wa upelelezi mkoa wa Dar es Salaam kamishna msaidizi wa polisi (ACP) Abdallah Zombe na askari wenzake watatu leo wamefikishwa mahakama ya Rufaa ambapo mwendesha mashitaka mkuu wa Serikali 'DPP' anapinga kuachiwa huru kwao baada ya kushinda mashitaka yaliyokuwa yakiwakabili ya mauaji. Mahakama ya Rufaa imesikiliza pande zote mbili na itatoa maamuzi baada ya majaji kupitia kesi yote.
Share on Google Plus

. Mtani

Mshana is Tanzanian blogger who writes different news without bias, He provides social, political and sports as well as Entertainment news happening in all parts around the World."STAY ME ALL THE TIME FOR INSTANT UPDATES.."
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment