mwanazuoni

SUMATRA DHIDI YA UDART NGOMA NZITO


Dar es Salaam. Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Majini na Nchi Kavu (Sumatra), imesema wakati wowote kuanzia sasa itaufikisha mahakamani uongozi wa Mabasi ya Kwenda Haraka (Udart) kwa tuhuma za kuwatoza abiria nauli zaidi kinyume na matangazo yao.
Mkurugenzi Mkuu wa Sumatra, Gilliard Ngewe alisema jana jijini Dar es Salaam kuwa, mashtaka dhidi ya uongozi huo yameshaandaliwa na kilichobaki ni kuyafikisha mahakamani.
Ngewe alisema Udart inatoza nauli ya Sh650 badala ya 400 kwa ruti ya kutoka Mbezi hadi Kimara na kuwatoza Sh650 nyingine kutoka Kimara hadi Posta.
Akizungumzia hilo, Mkurugenzi Mtendaji wa Udart, David Mgwassa alisema kama wana ushahidi waendelee na hatua yao ya mahakamani.
Share on Google Plus

. Mtani

Mshana is Tanzanian blogger who writes different news without bias, He provides social, political and sports as well as Entertainment news happening in all parts around the World."STAY ME ALL THE TIME FOR INSTANT UPDATES.."
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment