CHUACHUA CUP KUZINDULIWA LEO MASASI
Ligi iliyoanzishwa na Mbunge wa Jimbo la Masasi ndugu Dr Rashid Chuachua, inatarajiwa kuzinduliwa siku ya Leo katika viwanja vya Boman mjini Masasi na Mgeni rasmi atakuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana Wa Chama Cha Mapinduzi Wilaya ya Masasi ndugu Halfan Matipula.
Ligi hiyo itajumuhisha timu 14 Kutoka katika Kata za Halmashauri ya Masasi mji Lakini Changamoto iliyopo Kata ya Mtandi yakosa mwakirishi katika ligi hiyo.
Mshindi Wa kwanza Katika mchezo wa Mpira Wa miguu kwa wanaume ataondoka na zawadi ya Tsh 1,000,000/= na Mshindi Wa Pili ataondoka na Tsh 500,000/=.
Pia michuano hiyo itashirikisha timu Sita (6) za Mpira Wa miguu wa wanawake.
Na zawadi za Mpira Wa miguu wa wanawake zitakuwa Kama ifuatavyo :
Mshindi Wa kwanza - Tsh 500,000/=
Mshindi Wa Pili - Tsh 300,000/=
Mshindi Wa tatu - Tsh 200,000/=
Karibuni Kesho wadau wa Michezo kwenye Uzinduzi huo. Michezo inaleta Furaha na michezo ni ajira.
Kwa Hisani ya
Ofisi ya Mbunge Masasi.

Mtani
0 comments:
Post a Comment