TAMKO
LA KILIO CHA WANYONGE WA KAWE KUHUSU DIWANI CUP 2016
Kwanza kabisa nianze
kwa kumshukuru Mungu kwa kuweza unipa siha njema na kuweza kunipa uwezo wa
kushika kalamu na karatasi kuandika andiko ili la KILIO CHA WANGONGE WA KAWE KUHUSU DIWANI CUP 2016.
Pia nifaraja kwangu
kuona katiba ya nchi ya mwaka 1977 ibara ya 18(a) – (e) inanipa uhuru kwa
kufanya jambo hili. Asante Tanzania.
Kabla ya kwenda kwenye
nukta ambazo nimepanga kuzijadili japo kwa upana wake, napenda kuanza kwa
kuangalia maana ya uongozi na kiongozi. Maana ya Uongozi.
Uongozi
ni dhana, taaluma inayompa mhusika madaraka na uwezo wa kuwawezesha wale
wanaongozwa kuunganisha nguvu, stadi na vipaji vyao na kuvitumia ili kufikia
malengo yao.
Kuongoza
ni kujua lengo la wale wanaongozwa na njia ya kufikia lengo lao.
Tunaweza kuwagawa
viongozi katika mafungu yafuatayo kulingana na jinsi walivyoingia madarakani na
namna wanavyoongoza kama ifuatavyo:
a.
Wale wanaopata uongozi kwa kurithi.
b.
Wanaopata uongozi kwa kuchaguliwa na
watu
c.
Wanaojitwalia mamlaka ya kuongoza.
d.
Wanaoteuliwa na mamlaka za juu zaidi.
Uongozi
wa Kidemokrasia ni upi?
Uongozi
wa kidemokrasia ni ule wa kushirikisha watu katika
kufanya maamuzi na utekelezaji wake.
Sifa
za Kiongozi bora.
Kuna sifa nyingi za
kiongozi bora ikiwa pamoja na maadili, uaminifu, ufahamu n.k lakini mimi
najikita katika Maadili.
Maadili
: kiongozi ni lazima akubarike katika jamii anayoiongoza. Ili akubarike ana
budi kuzingatia maadili ya msingi ya jamii na taasisi zake. Kiongozi mwongo,
mlevi,mvivu, asiye mwaminifu n.k hawezi kuwa kiongozi.
Baada ya kuangalia za dhana
nzima ya uongozi japo kwa uchache. Ni muda wa kujadili kilio cha wanyonge
kuhusu Diwani Cup Kawe 2016. Nitajikita kwenye nukta kadhaa ambazo ni msingi wa
andiko languhili la wanyonge wa Kawe.
Ø Je tunamalengo ya kuleta Maendeleo
KAWE ?
Ø Je kazi ya Kiongozi kushirikisha na
kuunganisha nguvu kwa wananchi wake inafanyika ?
Ø Mashindano ya Diwani Cup Kawe
yalikuwa na dhamira ipi?
Kabla niseme
sitozungumzia kiingilio wala zawadi ina thamani gani? Nitazungumzia wananchi wa
KAWE wamepata athari zipi?. Kuna athari mbali mbali zimepatikana kutokana na
Mashindano ya DIWANI CUP KAWE kuwa
na Sura ya Kihuni. Jambo ambalo wapenda Maendeleo tunapinga kwa nguvu zote.
Athari tulizopata wanyonge wa Kawe na Wapenda Maendeleo ni kama ifuatvyo:
i.
Kutugawa
wanaKawe kwenye makundi mawili au zaidi.
Baada
ya mashindano haya kuisha katika sura ambayo imeleta mkanganyiko umepelekea
kutufanya sasa wanajamii kuwa na makundi mawili au zaidi. Hali ambayo katika
ustawi wa maendeleo ni hatari kubwa sana. Leo kuna watu kawe walikuwa marafiki awezi kuombana hata
maji lakini haya yamefanywa na wale ambao tumewapa dhamana ya kutuongoza tena
kwa njia ya kidemokrasia. Naanza kupata mashaka na kura yangu pia inanipa mashaka tena katika kuchagua
viongozi kipindi kijacho. Kawe tunaitaji umoja wetu uendelee lakini kwa kupitia
Mashindano ya Diwani Cup Kawe mmevunja Umoja wetu hii ni athari kubwa
iliyofanywa na watu wachache bila ya kuangalia maslahi ya umma na kuweka
maslahi yao binafsi mbele.
ii.
Kuharibu
taswira na heshima ya Kawe kwenye Uga wa Michezo.
Kawe
ni miongoni mwa maeneo yaliyojijengea sifa kubwa katika wilaya ya kinondoni
hasa kupitia mchezo wa mpira wa miguu. Nakumbuka kipindi kile bado nipo shule
ya msingi tulipokuwa tunakwenda msasani kwa miguu kuangalia timu za kawe
zilipokuwa zinacheza na kwa kweli Msasani Palikuwa panajaa endapo timu za kawe
zikicheza. Timu ambazo ziliipa sifa kubwa kawe kwa kipindi kile ni Ukwamani,
Kawe Ranger na Maskani Fresh. Mimi nilikuwa maskani fresh sikumbuki kwa nini
nilitokea kuipenda maskani fresh labda kwa kuwa walikuwa wanawachezaji wazuri. Nakumbuka
ila leo KIFA tumepeleka sifa mbaya sio sifa zile za mwanzo leo Kawe inaonekana
kuna viongozi wapiga dili ‘ matapeli’. Una hoja za msingi za kuvunja mashindano
kwa kufata sheria zako za mashindano kwa nini ukimbie wito wa KIFA? Mimi najiuliza
tu.
iii.
Kuwanyima
burudani Wanakawe
Huku ni kuwanyima
burudani wana Kawe. Kitendo hiki akikupaswa kufanywa au ndani yake kuwa na
kiongozi alipewa mamlaka ya kuwaongoza wananchi. Nakumbusha tu ….
kidogo Uongozi ni
dhana, taaluma inayompa mhusika madaraka na uwezo wa kuwawezesha wale
wanaongozwa kuunganisha nguvu, stadi na vipaji vyao na kuvitumia ili kufikia
malengo yao.
Kuongoza
ni kujua lengo la wale wanaongozwa na njia ya kufikia lengo lao
Lengo
la wana Kawe ni burudani hasa kupitia mpira wa Miguu lakini kiongozi unakuwa
katika kushiriki kuharibu burudani je unajua lengo la Uongozi? Hapa Mshana
Nauliza tu kwa nia ya kujenga.
Kwa
uelewa wangu wa majukumu ya KIFA na
Nguvu walizokuwa nazo za kisheria na kimamlaka wana Uwezo wa kufungia
mashindano kutofanyika KATA ya Kawe. Je wakifanya hivyo sisi tuende wapi? Leo Mshana
nikashuhudie mpira Kunduchi? Ninafaidika na nini kwa serikali kutuachia
kiwanja? Nifahamiana vipi na ndugu zangu wa mzimuni tukiwa pamoja. Moja ya
lengo la Mashindano yoyote yale duniani ni kuleta umoja na mshikamano. Viongozi
mnalakujibu juu ya dhuruma mnayotufanyia wanyonge wa kawe.
iv.
Kuua
vipaji vya wana Kawe Wanyonge
Lengo
lilikuwa lipi la kuanzisha mshindano la DIWANI
CUP KAWE 2016?
Mtanisaidia
waandaaji wa diwani cup . Hivi kwa mwenendo mbovu huu tunaweza kweli kukuza
vipaji au atujui thamani ya vipaji? Tunaua vipaji kwa gharama nafuu kwa kuweka
maslahi binafsi mbele.
Hizi ni athari na kilio
cha Wanyonge wa Kawe Kuhusu Diwani Cup.
Kwa nini haya
yametokea? Je yametokea kwa Bahati mbaya au yamepangwa? Nasema haya yametokea
kwa malengo maalumu ya Watu Fulani. Ithibati za kusema hivyo ninayo ila
najielekea kwenye sababu zifuatazo:
Sababu hizi zinaonyesha
na zinatufanya WANYONGE WA KAWE TULIE,
hizi sababu zimepangwa kwa kupitia maeneo haya kama ifuatavyo:
·
Viongozi
kuwa viashiria vya ukosefu wa maadili.
Waliokuwa wanaendesha
mashindano haya wanaonekana wazi kuwa wana viashiria vya ukosefu wa maadili. Kwa
nini nasema yawezekana wana viashiri vya ukosefu wa maadili kwanza nikumbushe
tena kidogo …. Maadili : kiongozi ni lazima akubarike katika jamii anayoiongoza. Ili akubarike
ana budi kuzingatia maadili ya msingi ya jamii na taasisi zake. Kiongozi mwongo,
mlevi,mvivu, asiye mwaminifu n.k hawezi kuwa kiongozi. Unakaa na
viongozi wa timu Fulani mathalani Kawe
Veterani na kukubaliana nao wasilipe kiingilio halafu kesho unawaambia
walipe ? una maadili ya uongozi kiongozi apaswi kuwa mwongo. Lakini anatokea
mtu anajitolea kuendeleza vipaji kwa kujitolea mipira kwa timu iliyoshinda wewe
uankwenda nayo kwako na watu wanapofata unaleta uswahili tena mbele ya mgeni
unajenga taswira gani ? na kiongozi wenye mamlaka ya kuwatumia wananchi
unashindwa kukemea , maadili yako ya uongozi yapo wapi? Kwa maana hiyo
yaliyotokea yamepangwa na kubarikiwa na uongozi.
·
Zawadi
ya mshindi kutolewa nyumbani kwa mwanzilishi wa mashindano.
Sijawahi kusikia wala
kuona sehemu nyingine duniani ispo kuwa Kawe Yetu. Leo nilikuwa napitia nyaraka
mbalimbali na kupitia documentary za waanzishi wa mashindano ya mpira wa miguu
na mashindano mengine duniani nimeshindwa kupata kuona zawadi ikitolewa kwa
mtindo huu. Kwa ambaye amewai kuona au kusikia nje ya Kawe naomba anitumie
kupitia email yangu halfanm8@gmail.com kama ana
video anitumie whatsapp kwa namba hii 0712474810. Nina kila sababu ya kusema
kuwa yaliyotea yana Baraka zote za Uongozi na yalipangwa.
Nina mengi ya kusema
Mnyonge mimi na wezangu Poleni Wanyonge Wezangu Tufute machozi na tumlilie
Mungu kwa Kusema Yana Mwisho Haya Yote kwa Uwezo wake. YATATIMIA
MSHANA B. HALFAN
MSEMAJI WA WANYONGE WA KAWE
06.12.2016
MASASI.
0 comments:
Post a Comment