mwanazuoni

Punguzo la kodi litaleta nafuu: Donald Trump

Rais Donald Trump ametangaza kile anachokiita punguzo kubwa la kodi kuwahi kutokea katika historia ya taifa hilo. Amesema anahitaji mfumo rahisi na wa wazi wa kodi ili kurejesha ajira na utajiri ndani ya taifa hilo.
Trump ametangaza kupunguza kodi kwenye biashara na amesisitiza kuwa ataondoa kodi ya urithi. Amesema wafanyakazi wanawake kwa wanaume ndiyo watakao nufaika na hatua yake hiyo na si wale wenye mapato makubwa.
"Mfumo wetu mpya unalenga mabadiliko ambayo,yatamlinda mtu wa kipato cha chini , cha kati na katika ngazi ya kaya siyo kwa matajiri.
Wataniita kwa majina yoyote wapendayo, lakini haitasaidia. Ninafanya mambo ya haki na si kwa manufaa yangu mwenyewe.Naomba mniamini."
Hatua hii ni kutekeleza mapendekezo ya chama chake cha Republicans, huku Democrats wakiwa na maoni tofauti kwamba mabadiliko hayo yataziumiza familia zenye kipato cha kati na kupunguza kipato chao hasa wajane na watoto.bbc
Share on Google Plus

. nyumbanitz

Mshana is Tanzanian blogger who writes different news without bias, He provides social, political and sports as well as Entertainment news happening in all parts around the World."STAY ME ALL THE TIME FOR INSTANT UPDATES.."
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment