mwanazuoni

Wazazi wa Warmbier waeleza mateso yaliomkabili Korea kaskazini

Wazazi wa Otto Warmbier wameelezea hali ya kutisha iliomkabili mtoto wao alipowasili nyumbani kutoka Korea kaskazini.
Fred na Cindy Warmbier wameliambia shirika la habari la Fox and Friends kuwa Watu wa Korea kaskazini ni "magaidi waliomtesa mtawalia" mtoto wao.
Mwanafunzi huyo wa Marekani alifungwa Pyongyang mnamo 2016 kwa kuiba kibandiko cha hoteli.
Aliachiwa kwa misingi ya matibabu mnamo Juni mwaka huu lakini aliwasili nyumbani akiwa mahututi na alifariki siku chache baadaye.
Korea kaskazini imekana daima kumtesa Warmbier. Inasema aliugua bakteria ya neva mwilini lakini madakatari wa Marekani hawakugundua bakteria yoyote.
'Hii haikuwa ajali'
Katika mahojiano yao ya kwanza tangu kufa kwake, wameliambia shirika la habari la Fox news kwamba "wanahisi umewadia muda kusema ukweli kuhusu hali iliyomkabili Otto".
Madakatari Marekani walisema alikuwa katika hali ambayo mwili wake ulikuwa hauitikii, lakini familia ya Warmbiers wanasema kuita hali hii coma "sio haki".
Bi Warmbier anasema walipomuona mtoto wao alikuwa "anazunguka na kufafatika kwa nguvu akitoa sauti isiyo ya binaadamu"bbc
Share on Google Plus

. Mtani

Mshana is Tanzanian blogger who writes different news without bias, He provides social, political and sports as well as Entertainment news happening in all parts around the World."STAY ME ALL THE TIME FOR INSTANT UPDATES.."
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment