mwanazuoni

UNAFIKI WA MHE. MBOWE KATIKA MAMBO MUHIMU

UNAFIKI WA MHE. MBOWE KATIKA MAMBO MUHIMU


Kwanza kabisa napenda kuwashukuru wale wote ambao walitumia muda wao kupitia na

kudurusu makala yangu iliyokuwa na kichwa cha habari kisemacho " WATANZANIA TUITAZAME

CHADEMA KWA JICHO LA TATU" Makala hiyo ilichapwa tarehe 12-02-2014 siku ya jumatano.

Ni makala ilichangiwa na watu wengi na kupokea maoni na ushauri kuliko makala zangu

zote ambazo nimewahi kuziandika hapo nyuma. Ila waswahili wanasema kuwa "kwenye

wengi hapakosi jambo"
hivyo nilipokea maoni tofauti na ushauri lakini pia

nilipokea maneno yenye lugha chafu ila nimechukulia kama changamoto za walimwengu tu.

Mimi nasema kuwa wale wote waliotumia lugha chafu hawajui walitendalo na mimi
nimeshawasamehe.

Nimetoa utangulizi na sasa ni wakati mzuri kwenda kwenda katika kile ambacho

nimekusudia watu mbalimbali wapate kukijua japo kwa kutumia muda wao mchache katika

kudurusu haya machache ambayo ni mawazo yangu binafsi. Nasawishika leo kuandika

makala hii ambayo nitamzungumzia kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni pia ni

mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo kwa kifupi CHADEMA.Kimsingi kuna

sababu mbalimbali ambazo zimenishawishi kuandika makala hii ila kubwa zaidi ni

mwenendo wa kiongozi wangu ambaye ni miongoni mwa watu wenye ushawishi mkubwa kwa

wanajamii wa kitanzania, hivyo watanzania wezangu wasipomjua vizuri itakuwa ni hasara

kwa taifa kwani watajikuta wamepata hasara kubwa katika taifa ili masikini.

Kabla ya kuingia katika kusudio la makala hii ni vema kumjua japo kwa ufupi historia

yake kama ifuatavyo:

Jina lake ni Freeman Aikaeli Mbowe, amezaliwa 14 septemba, 1961 mkoani Kilimanjaro na

elimu yake ni ya sekondari tu kwani alisoma katika shule ya uhungo seminari iliyopo

Bukoba. pia ameoa mke ambaye ni mtoto wa mwasisi wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo

anayeitwa Lilian E. Mtei , Mhe. Mbowe amebahatika kuwa na watoto Sita na kwa sasa

anamke mwingine ambaye ni mke wa kisheria ambaye ni Joyce Mukya na kubahatika kupata

mtoto moja. Kuna watu watajiuliza Mhe. Mbowe ni mkristo itakuwa je awe na mke

mwingine hapa nitafafanua kwa uchache tu. Kumbuka sheria zinasema ukikaa na mwanamke

kwa miezi inayozidi sita unahesabika kuwa umeoa. Mhe. Mbowe bila ya kuhesababu huko

nyuma wamekuwa wapenzi kwa muda gani tuhesabu hapa kuanzia mimba mpaka kuzaa miezi

mingapi imepita ? je aijakamilika sita ya kisheria? najua kila mtu ambaye

atakishughulisha kichwa chake atakuwa amepata jibu la swali hilo.

Kwa sasa Mhe. Mbowe anajushughulisha na siasa pia ni mwenyekiti wa Chama Cha

Demokrasia na Maendeleo.

Mwaka 2000 alichaguliwa kuwa mbunge wa jimbola Hai ambalo alishinda kwa asilimia

64.5% za kura zote zilizopigwa, vile vile kutokana na ushindi ambao aliupata mwaka

2000 alitumia haki yake kikatiba na kujua kuwa watanzania wa Hai ni sawa na

watanzania wa nchi nzima akahamua kujitosa katika kugombea nafasi ya urais mwaka 2005

kukiwakilsha chama chake cha CHADEMA. Tarehe 14 Decemba, 2005 alipata asilimia 5.88%

ya kura. Baada ya matokeo hayo mimi kwa uwezo wangu nilijaliwa na mungu niliamini

kuwa mtoto akizaliwa uanza kukaa na kuendelea kutamba na mwisho kutembea lakini ni

tofauti na Mhe.Mbowe yeye alitambaa pia akatembea mwisho wa siku akarudia kutambaa

haya ni maajabu ya ulimwengu huu. hapa nina maana kuwa mwaka 2000 aligombea ubunge na

mwaka 2005 aligombea uraisi lakini cha ajabu mwaka 2010 alirudi kugombea ubunge kwa

mimi naona ni maajabu sijui wewe mwezangu? mwaka 2010 aligombea ubunge na kumshinda

mgombea wa CCM ndugu FUYI KIMBITA kwa asilimia 51.63% ya kura. hapa unaona ni jinsi

gani ameshuka kutoka asilimia 64.5 % mwaka 2000 na kufikia asilimia 51.63% matarajio

yangu mwaka 2015 atapata zile asilimia alizopata katika urais hii itatokana na

mwenendo wake wa sasa wa kiongozi huyu.

Baada ya kuwapatia machache na historia yake japo kwa ufupi ili wewe msomaji wa

makala hii uweze kujua ni nani anazungumziwa hapa na niwapi katoka mpaka kufikia hapa.

Swali ni kwa nini mwandishi wa makala amehamu kuandika hii makala yenye kitambulisho

cha " UNAFIKI WA MBOWE KATIKA MAMBO MUHIMU" kimsingi kuna sababu nyingi mno

zilizomshawishi mwandishi kuandika makala hii ila nitazitaja chache kutokana na wingi

wake ila mungu akipenda zitakuja kuzitaja nyingine katika makala nyingine pale tu

mwandishi atakapo pata wasaha wa kufanya hivyo, ila kwa uchache tujilizishe na hizi

zifuatazo:

A. UFISADI MKUBWA UNAOFANYWA NA MHE. MBOWE.


Mhe. Mbowe ni kiongozi mnafiki pale anapozungumzia suala la ufisadi kwa kuwa na yeye

ni fisadi mkubwa kwa msamiati huu niliupata kwa Bw Mengi ila mimi nitautumia kwa Mhe.

Mbowe kuwa naye ni fisadi papa. Hapa namnasibisha na Chui alivaa ngozi ya Kondoo.

Mhe. Mbowe ni fisadi papa na hapa nitaweka baadhi ya ithibati za kuthibitisha ufisadi

wake, kwa kuanza nitaanza na kumnukuu kiongozi mwenzie mwenye nafasi ya juu ndani ya

CHADEMA alipotamka haya maneno hivyo ni ithibati namba moja

" Nadhani alimwambia pia mwaka 2008 ( Baada ya orodha ya mafisadi

kutangazwa2007)Mkono alimpa Freeman Aikaeli Mbowe shilingi Million 20 za uchaguzi

mdogo wa Tarime na Freeman akasema kwenye chama ametoa mkopo na akalipwa
"

Ni nukuu ya Zitto Kabwe katika profile yake ya Facebook.

Je huu si ufisadi? amepokea pesa kutoka kwa mtu kisha anakuja katika chama anasema

kuwa amekikopesha chama pesa na kushindikiza kulipwa na akalipwa huu ni ufisadi.

hivyo mtu huyu anapozungumzia ufisadi ni unafiki ulitukuka.

Pia chanzo cha taarifa kiliendelea kutoa data za ndani ambazo ni ithibati ya pili ya

ufisadi wa Mhe. Mbowe "Nadhani alimwambia pia mwaka 2010 Mkono alimpa Mbowe

Millioni 200 za kampeni ya Slaa pia hakusahau kumwambia kuwa Rostam Azizi alimpa

Mbowe Sh million 100 za kampeni. Lissu anajua ? "


Kwa maelezo hayo ya naibu katibu mkuu wa chama taifa ni ithibati tosha za

kuthibitisha kuwa Mbowe ni fiasdi papa ambaye ni mnafiki aliyetukuka na pale

anapokuwa anataka kuwaaminisha watanzania kuwaona kuwa CCM peke ndio mafisadi hali ya

kuwa naye ni miongoni mwa mafisadi huu ni unafiki uliyovuka kiwango yaani ni unafiki

ulitukuka. basi si hayo tu bali kuna ithibati nyingine ambayo inaonyesha kuwa

Mhe.Mbowe ni fisadi papa ni huu hapa chini ebu soma kwa makini halafu tafakari kwa
kina


" Kufuatia uchaguzi mkuu wa mwaka 2005, Mhe. Mbowe alitufahamisha wanachama kuwa

alikuwa anakidai chama US $ 181,949.00 sawa TSH 218.338,546. Mpaka sasa chama

kimekwisha mlipa TSH 175,000.000/= Baada ya kupata wadhifa wa makamu Mwenyekiti na

kwa kuzingatia takwimu zionekanazo hapo juu katika kulinganisha matumizi ya fedha

wilayani na makao makuu niliamua kumshauri Mbowe asitishe kujilipa deni kutokana na

fedha za ruzuku kwani siamini kuwa kulipa madeni yaliyopo kwa kuendana na utaratibu

wa usimamizi wa fedha za ruzuku kwa vyama vya siasa toka serikalini.

Mhe. Mbowe alichachamaa na ndipo nilipomshauri kuwa kama ni hivyo basi atuthibitishie

pesa hizo anazodai chama aliko[esha chama ziliingia kwenye akaunti gani ya chama

yaani CHADEMA, KUPITIA HUNDI ipi na lini? nilimuomba pia kutaja ni kikao gani cha

chama kiilihidhinisha matumizi ya fedha hizo kwani kama hakuna ushahidi wa

maidhinisho ni dhahiri kuwa matumizi hayo haykuthibitishwa na chama na kwa mantiki

hiyo kuyafanya kuwa matuumizi binafsi ya Mhe. Mbowe. V ile vilenilimueleza kuwa

yalikuwa yakinukia harufu ya Ufisadi.


Stakabadhi zote kuhusiana na matumizi hayo zilionesha kuwa gharama za aidha ununuzi

na au ukodishaji wa vifaa hivyo, hazikutofautiana na viwango wanavyolipishwa watalii

kwa huduma kama hizo, kwa maana ya gharama ya juu sana. nNa kwa kuwa hata baada ya

kuwa Mhe. mbowe amekwisha lipwa zaidi ya nusu ya deni alilodai kuikopesha CHADEMA

VIFAA VYOTE YAKIWEMO MAGARI, VIPAZA SAUTI NA KADHALIKA VIMEBAKIA KUWA MALI YAKE

BINAFSI, basi bila kumficha nilimueleza kuwa huko ni kukinyonya chama kwa kukigeuza

kitega uchumi cha watu binafsi. Kuhusu suala la kulipa madeni kupitia ruzuku ya

serikali, nilimuomba Mhe. Mbowe afuatilie kwa Msajili wa vyama kweli fedha za ruzuku

ya serikali kwa vyama vya siasa, inaweza kutumika kulipia madeni ya viongozi wa vyama

hivyo yatokanayo na uchaguzi ili CHADEMA isiathirike kisheria. Nimesema kweli hapa

kwamba kwa wanachadema wengi walinichagua kuwa makamu mwenyekiti na hata mimi

mwenyewe tulikuwa wagombea wa nafasi ya ubunge,udiwani n.k katika uchaguzi wa mwaka

2005 ningeferijika sana iwapo na sisi tungerejeshewa angalau chochote cha kufidia

gharama zetu, kwa maana kwamba kama chama kimeamua kurudisha gharama hizo kiwalipe

wote baada ya kulipa madeni kwa wateule wachache "



Je kuna shaka lolote nikisema kuwa Mhe. Mbowe ni fisadi papa ? hakuna shaka kwani kilakitu nimeweka wazi kupitia nukuu za viongozi wakubwa ndani ya chama cha

Demokrasia na Maendeleo. Kwa kudurusu baadhi ya maandiko tu hayo hapo juu tumeiona

ufisadi mkubwa unaofanywa na Mhe. Mbowe, swali la kujiuliza hapa tumempa taasisi

ndogo kama Saccos ameweza kufanya ufisadi wa kutisha kwa namna hii. Je, tukimpa nchi


au wizara ya fedha nchi itakuwa katika hali gani?

B. KUWAIBIA WANYONGE WA NCHI HII( UMMA UNATEKETEA KWA UNAFIKI WA MBOWE)


Napenda kuchukua nafasi adhimu ya kuwatazalisha ndugu zangu watanzania wezangu wenye

uzalendo na nchi hii kuwa makini na kiongozi huyu aliyevaa ngozi ya Kondoo angali

yeyey ni Chui mkubwa. Nchi hii ikiwa inajitaidi katika kupambana na maharamia wa

kigeni kumbe inasahau kuwa kuna maharami wanyeji ambao wamekuwa mwiba wa maendeleo ya

uchumi wetu ambao wanatumia nyadhifa zao katika kuwaibia wanyonge wa nchi hapa pia

nina mifano dhahiri ambayo ni ithibati tosha kuwa Mhe. Mbowe ni mnafiki katika mambo

muhiu ya taifa ili.

" aeleze aliingia deal gani na Kinana na Sumaye mwaka 2005 kuifutia deni lake la NSSF. Aweke wazi mikataba yake na NHC kuhusu nyumba ya Umma ilipo Club Bilicanas"

Ebu tazama ni jinsi gani huyu jamaa alivyokuwa nafiki ambaye hata athamini kazi

iliyofanywa na watanganyika walitukomboa katika unyonyaji wa watu weupe. Je maesahau

mchango wa wazee wangu hakina Abdulwahd Syjes, Osca Kambona,Bibi Titi Mohammed,J.K wa

Kwanza, Dossa Azizi, Mwalimu Kiyele,Mzee Mtevu na sheik Amiri na wengine wengi ambao

walitumia muda wao mwingi kuhakikisha mtanganyika anatoka katika unyonyaji wa namna

yoyote lakini leo mtanzania mwenzetu anaturudisha katika karne ya ukoloni kwa kutumia

rasilimali zetu kujinufaisha binafsi huu ni unyonyaji kwani NHC NA NSSF ni mali ya

wanyonge wa nchi hii. Pia kuwafanya watanzania kutopa mahitaji yao ya msingi kwa

kuendekeza tamaa zake ni kuwanyonya wanyonge wa nchi hii ebu soma hapa "

amemshinikiza mbunge wa viti maalumu ndugu Joyce Mukya, kukatisha ziara ya kikazi za

kibunge alipopangiwa na kumlazimisha wakutanane nyumbani kwake Dubai"


ushahidi wa ili ni hizi sms " bwana kabunju, salaam. Rejea mazungumzo kuhusu

Mhe.Joyce Mukya ambaye yuko safarini . Nitashukuru akibadilishiwa booking yake aweze

kuondoka New York Tarehe 1 Dec siku ya jumapili kurejea Dubai na kuunganisha Dar tar

3Dec. Mbowe,KUB.Cc Mhe.Joyce Mukya"


Huyu ni mtanzania mwenzetu ambaye anachukua mpaka kile kidogo chetu.

Pia wanyonyaji weusi wamekuja na mbinu mpya ya M4C yaani ni Movement for Change

ambayo kimsingi ni miongoni mwa mbinu ya unyonyaji kwa wanyonge wa nchi hii ambayo

mimi nainasibisha na mbinu zilizokuwa zinatumika katika kipindi cha feudalism

(ukabaila) pale Feudal lord(kwa sasa ni Mbowe) walipokuwa wanawatumia wakulima

katika kujipatia kipato chao bila hata jasho lakini leo hawa feudal lord wanawatumia

maskini wa nchi hii katika kujipatia kipato chao kwani tofauti ya feudal lord wa

karne ya 18's na hawa wa karne ya 21 ni moja tu kwani feudal lord walitumia

ardhi(land) lakini hawa wa sasa wanatumia M4C( Movement for Change ).


C. KUKIFANYA CHAMA KUWA MRADI WAKE BINAFSI
Mwenendo wa uendeshaji wa chama cha CHADEMA kwa sasa hakuna tofauti na uwendeshaji wa

biashara fulani nahisi sitokuwa nimekosea nikapo sema ni saccos kwa sababu mbalimbali

moja kuwa chama cha siasa kinaendeshwa kwa msingi wa kidemokrasia lakini saccos

inaendeshwa kwa msingi wa mmiliki je kuna tofauti na chadema ya Mbowe kwani yeye

anaiendesha jinsi anavyotaka. Hapa najua watanzania makini watakuwa wamenielewa kwa

wepesi kwani wengi wetu tunajihusisha na saccos pia nina ushahidi wa uwazishwaji wa

chama cha chadema. Ila kwa leo si lengo langu juu ya ili ilaitakapotakiwa nitakuja

kuchambua kila chama kilivyoanza ili watanzania wajue kwa nini nainasibisha CHADEMA

na SACCOS. Mhe. Mbowe amefanya chama ni mradi wake juu ya ushahidi wa ili nakuomba

rejea walaka wa Chacha Wangwe ambao umeelezewa katika hoja iliyopo katika kifungu "A"

cha makala hii.


D. KUTUMIA PESA NYINGI KUWATHIBITI WALE WOTE AMBAO NI WANADEMOKRASIA YA KWELI
Je Mhe. Mbowe si mnafiki? leo ukiniambia kuwa kiongozi huyu ni mzalendo na

mwanaDemokrasia napata mashaka na weledi watu ambaye atareta hoja ya namna hiyo kwa

sababu mbalimbali ikwemo juu ya mwenendo wake. Kuna mifano mingi sana ambayo

inathibitisha kuwa Mbowe si mwanademokrasia pia mnafiki aliyetukuka katika mambo

muhimu kwani ebu tureje mambo ambayo yamefanya Ndugu zangu Habibu Mchange, Mtela

Mwampamba, Samson Mwigamba,Dr Kitila Mkumbo,Marehemu Chacha Wangwe na Juliana Shonza

kuwa nje ya Chadema ? kuna watu watajito ufahamu kwa kufanya hawajui basi hata la

Mhe. Kafulila? sawa basi ili la juzi ambalo limefanywa kuwa kiboro la Mzalendo Zitto

Kabwe nalo tumelisahahu?



Nina mengi sana ila kwa kuwa muda na mambo ya kijamii yamekuwa nayo yakidai mudA

kutoka kwangu basi naoma nishie hapa ila natoa ahadi ya kuja kumalizia makala hii

wiki ijayo kwani itakua na muendelezo wa makala hii. Nakuomba msomaji wangu usikose

kusoma muendelezo wa makala hii.

Kwa maoni na Ushauri , tumia njia hizi za mawasiliano kwa mwandishi
Jina : MSHANA Junior
SIMU :0712 47 48 10
BARUA PEPE : halfanm8@gmail.com

Share on Google Plus

. Mtani

Mshana is Tanzanian blogger who writes different news without bias, He provides social, political and sports as well as Entertainment news happening in all parts around the World."STAY ME ALL THE TIME FOR INSTANT UPDATES.."
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment