mwanazuoni

SHEIKH PONDA AENDELEA KUTESEKA GEREZANI BAADA YA RUFAA YAKE YATUPILIWA MBALI.

Ukaguzi mkali kwa kutumia kifaa maalumu ukifanyika katika mlango wa kuingilia Mahakama Kuu.
MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam, jana imetupilia mbali rufaa ya Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh Issa Ponda iliyopelekwa na wakili wake Juma Nassoro ya kupinga hatia ya adhabu aliyohukumiwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu akidai kuwa hapakuwa na ushahidi wa kutosha wa kumtia hatiani kwa mashtaka yaliyokuwa yakimkabili.
Kesi nyingine ya uchochezi inayomkabili kiongozi huyo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ambayo inasikilizwa na Jaji Augustine Shangwa imeahirishwa hadi Novemba 20, mwaka huu.
(Picha na Haruni Sanchawa/GPL)

Wafuasi wa Ponda wakiimba nyimbo mbalimbali nje ya mahakama.

Dola ikifanya mawasiliano kuimarisha ulinzi.


Magari ya Askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) yakiwa yametanda eneo la mahakama.

Share on Google Plus

. Mtani

Mshana is Tanzanian blogger who writes different news without bias, He provides social, political and sports as well as Entertainment news happening in all parts around the World."STAY ME ALL THE TIME FOR INSTANT UPDATES.."
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment