mwanazuoni

SIKU 48 ZA MBUNGE WA MASASI KULETA MAENDELEO JIMBONI



Ubunge ni kazi ya wito katika kuwatumikia wananchi  kwa lengo la kuleta maendeleo na usawa wa  haki katika jamii husika. Na kwa kawaida kiongozi mzuri ni Yule anayefahamu matatizo ya watu wake na kuyafanyia kazi kwa wakati mahsusi bila ya kusubili kuambiwa.
Kwa kulitambua hilo mbunge wa  Masasi Ndugu Dr Rashid Chuachua Jana alifanya mkutano wake wa kwanza katika kata ya Mkuti na wapili tangua achaguliwe kuwa mbunge  wa jimbo hilo la Masasi. Kwa siku zake 48 za Ubunge ameweza kungundua changamoto mbalimbali ndani ya jimbo lake hilo na ameanza kuchukua hatua mbalimbali kuhakikisha anaondoa changamoto hizo.
Suala la Elimu
Mbunge kwa kutambua mchango wa elimu katika jamii yeyoyote ile katika kuleta maendeleo katika jamii. Ameweza kufatilia suala la madeni ya walimu pia ni miaka kadhaa sasa serikali aijapeleka walimu wa shule za msingi hivyo kuna uhaba wa walimu 219. Ila amefanya mazungumzo na waziri husika na ameaindiwa kupatiwa walimu wote 219 na serikali kwa mwaka wa fedha 2016/2017.
Changamoto za afya katika hospitali ya Mkomaindo.
Kuna changamoto nyingi sana katika hospitali ya Mkomaindo. Kwa kutambua umuhimu wa afya mbunge amefanya ziara kabla ya kuapishwa kuwa mbunge na kungundua changamoto mbalimbali zikiwemo ukosefu wa viafa tiba, shuka,  upungufu wa dawa na pia uhaba wa wauguzi katika hospitali hiyo.
Hivyo mbunge alianza kwa kutoa shuka 690 kwa ajili ya wagonjwa.
Pia Changamoto ya kukosa kituo cha afya , hivyo mbunge kushirikiana na mganga mkuu wanaandaa utaratibu wa kuhakikisha wanaborosha zahati ya mkuti.
Kifupi mbunge aligusia sehemu zote ambazo ni kero kwa wananchi wa jimbo lake pia aliambatana na wakuu wa Idara zote za Halmashauri ya Masasi pia wakiwemo madiwani na Mwenyekiti wa Halmashauri kwa lengo la kujibu kero za wananchi na kutolea ufafanuzi juu ya maswala ambayo ni vikwazo vya maendeleo mbele ya jamii husika. 
















 MWANANCHI AKITOA KERO YAKE KUHUSU TAKATAKA




 Ndugu Pascal Mratibu CHF akitoa maelezo kuhusu CHF




 Wananchi wakifatilia mkutano


 Mbunge akibadilishana mawazo wa mwenyekiti wa Halmashauri

 Mbunge akiandika swali liloulizwa


 MGANGA MKUU AKITOA ELIMU YA MFUKO WA AFYA WA JAMII

 Afisa wa Maji akielezea Mikakati



 Mbunge akipasua jipu la Chama cha Ushirika MAMCU akiwataka TAKUKURU Kufanya Uchuguzi wa Kina

 Mbunge Dr Chuachua akimuagize Mganga mkuu wa Hospital ya Mkomaindo kufatilia waliokuwa wanagawa Neti na Kuwauzia wenye Nyumba za Kulala wageni badala ya kuwapa wananchi hili wachukuliwe hatua

 wananchi wakifatilia mkutano

 Diwani wa Mkuti Ndugu Nachuma(chadema)

KATIBU WA MBUNGE

Share on Google Plus

. Mtani

Mshana is Tanzanian blogger who writes different news without bias, He provides social, political and sports as well as Entertainment news happening in all parts around the World."STAY ME ALL THE TIME FOR INSTANT UPDATES.."
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment