mwanazuoni

NAIBU SPIKA AZUA SINTOFAHAMU BUNGENI


 Naibu Spika wa Bunge, Dk. Tulia Ackson, Alhamisi hii amezua sintofahamu bungeni baada ya kumwita bwege Mbunge wa Kilwa Kusini, Seleman Bungara (CUF).

Dk. Tulia alimwita bwege mbunge huyo wakati wa kuchangia mjadala wa hotuba za bajeti za Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) pamoja na Utawala Bora.
Kilichomponza mbunge huyo ni hatua yake ya kusimama na kuhoji Bunge kutorushwa moja kwa moja kwenye runinga wakati Naibu Spika akitoa ufafanuzi kwa wabunge kuhusu mjadala uliokuwa ukiendelea.
“Bwege acha ubwege wako hapa… Bwege acha ubwege,” alisema Dk. Tulia huku akionya hatua ya kuzomea ndani ya Bunge.
Baada ya Dk. Tulia kutoa kauli hiyo, mbunge huyo alimjibu kwa kusema si ajabu kumwita bwege kwa sababu hilo pia ni jina lake.
“Bwege ndiyo jina langu, kwani kuna ajabu gani, kwani wewe mwanamume? Ukiitwa mwanamume utajisikiaje?” alisema mbunge huyo ambaye ni maarufu kwa jina la ‘Bwege’.
Hivi karibuni, mkazi wa Mtaa wa Olasit jijini Arusha, Isaac Habakuk Emily, alifunguliwa mashtaka na Jamhuri akidaiwa kuweka kwenye ukurasa wake wa Facebook ujumbe ulioonyesha kumdhihaki Rais John Magufuli kwa kumwita bwege, huku akijua kufanya hivyo ni kosa kisheria.
Ujumbe huo ulisomeka: “Hizi siasa za maigizo, halafu mnamfananisha huyu bwege na Nyerere wapi buana”.
Source:Mtanzania
Share on Google Plus

. Mtani

Mshana is Tanzanian blogger who writes different news without bias, He provides social, political and sports as well as Entertainment news happening in all parts around the World."STAY ME ALL THE TIME FOR INSTANT UPDATES.."
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment