mwanazuoni

MGOGORO HUU UTALETA MATOKEO MABAYA SIMBA SC

Katibu wa tawi la Simba (Ngurumo za Simba) Felix Makau amemtuhumu makamu mwenyekiti wa Simba Geoffrey Nyange ‘Kaburu’ kuwa ni mamluki wa Yanga kutokana na Kaburu kudai kutomtambua Mzee Hamisi Kilomoni kama mmoja wa wadhamini wa Bodi ya wadhamini wa klabu ya Simba.
“Mimi namjua Kaburu ni mamluki tu wala hana uchungu na Simba, yule ni Yanga. Akome kumdharau mzee Kilomoni,” maneno ya mzee Makau baada ya kutoka Ikilu kupeleka malalamiko ya Bodi ya wadhamini kupinga mchakato wa mabadiliko ya undeshwaji yanayotaka kufanywa na klabu ya Simba.
“Namshangaa hata huyu Kaburu Nyange anasema eti hamtambui Mzee Kilomomi mimi nahisi huyu kazaliwa Tandale na wale kwa wale watu wasiokuwa na baba, kama kweli anababa hawezi kumdharau mzee Kilomoni, kama yeye hana baba sisi tunababa zetu.”
“Mzee Kilomono kapata uongozi akiwa mchezaji wa Sunderland na ndiye aliyeanzisha ule mfumo wa wachezaji kujinyima posho ili kujenga klabu.”
Kutokana na mkutano mkuu wa dharura uliofanyika mwishoni mwa juma lililopita, Bodi ya wadhamini ya klabu ya Simba December 16 walipiga hodi Ikulu wakiongozwa na Mzee Hamisi Kilomoni kupeleka malalamiko yao ya kupinga mabadiliko ya uendeshwaji wa klabu hiyo.
“Kundi la marafiki wa Simba wanataka kuipoka Simba, nimeona kwenye vyombo vya habari wanasema MO katoa milioni 150 kuwapa wachezaji, ni uongo na propaganda. MO anawatega hawa wenzake wahuni kwamba anawakopesha lakini hili ni genge lao wanataka kujinufaisha wao wagawe hisa, tunaiomba serikali kuingilia kati, ndio maana tulienda Ikulu kwenda kumuona mheshimiwa.”
Mzee Makau anasema hawakufanikiwa kuonana na Rais badala yake walionana na wasaidizi wake ambao waliwasaidia kuwapa miongozo na anaimani watafanikiwa.
 
Share on Google Plus

. Mtani

Mshana is Tanzanian blogger who writes different news without bias, He provides social, political and sports as well as Entertainment news happening in all parts around the World."STAY ME ALL THE TIME FOR INSTANT UPDATES.."
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment