mwanazuoni

Trump aitaka China kuhifadhi manuwari ya Marekani


Rais mteule wa Marekani Donald Trump ,amesema kuwa Marekani inafaa kuiomba China kuiweka manuwari ya Marekani iliopatikana katika bahari ya kusini mwa taifa hilo.
Awali Trump alikuwa ameishutumu Beijing kwa kuiba manuwari hiyo katika maji ya kimataifa.
China iliichukua manuwari hiyo katika pwani ya Ufilipino wakati meli za wanamaji wa Marekani zilipojaribu kuichukua, hatua ilioikasirisha Marekani.
Beijing imesema kuwa itaikabidhi Marekani, lakini matamshi ya Trump huenda yakatatiza mpango huo.
Hii ni mara ya tatu katika wiki kadhaa kwa yeye kukosana na China.
Wakati huohuo Trump amekamilisha ziara yake ya wiki tatu ya kusherehekea ushindi , katika mji ulioshuhudia mkutano mkubwa zaidi wakati wa kampeni zake.
 
Alipowasili katika mji wa Mobile, Alabama, Trump alikaribishwa na kundi la wanawake waliovalia mavazi ya kitamaduni yanayovaliwa na jamii za kusini mwa Marekani.
Katika uwanja uliojaa pomoni, Trump aliahidi kwamba atatimiza ahadi yake ya kujenga ukuta kwenye mpaka wa Mexico na Marekani.
Trump ataapishwa tarehe 20 mwezi Januari.bbc
Share on Google Plus

. Mtani

Mshana is Tanzanian blogger who writes different news without bias, He provides social, political and sports as well as Entertainment news happening in all parts around the World."STAY ME ALL THE TIME FOR INSTANT UPDATES.."
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment