mwanazuoni

HTMAE LIBYA KUUNDA SERIKALI YA UMOJA


Kiongozi wa serikali ya Libya inayotambuliwa kimataifa, Abdullah al-Thinni amesema ana matumaini ya kutia saini ya makubaliano ya kugawana madaraka na wapinzani wake wa kisiasa.

Al-Thini amesema ana matumaini ya kufikiwa makubaliano katika awamu nyingine ya mazungumzo ya amani yatakayofanyika nchini Morocco siku ya Ijumaa.
Hali ya usalama nchini Libya imekuwa tete tangu wanamgambo walipoudhibiti mji mkuu wa nchi hiyo,Tripoli, mwaka jana na kuweka Bunge lao.
Al-Thini ni Waziri mkuu katika Serikali iliyoweka makao yake katika eneo la mashariki ya mji wa Tobruk.
Mjumbe maalum wa Umoja wa mataifa nchini humo amekuwa akifanya jitihada za kuhakikisha kuwa pande hizo mbili hasimu zinaunda Serikali ya umoja wa kitaifa.

chanzo : bbc swahili
Share on Google Plus

. Mtani

Mshana is Tanzanian blogger who writes different news without bias, He provides social, political and sports as well as Entertainment news happening in all parts around the World."STAY ME ALL THE TIME FOR INSTANT UPDATES.."
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment