mwanazuoni

PICHA YA MWANAMKE MTUMWA YAWEKWA KWENYE DOLA YA MAREKANI

Picha ya mtumwa mmoja aliyekata nyororo na kisha kusaidia mamia ya wenzake kutoroka utumwa sasa itatumika katika noti mpya ya dola 20 nchini Marekani.
Bi Harriet Tubman atakuwa Mwafrika Mmarekani wa kwanza kuangaziwa kwenye sarafu ya Marekani.
Vilevile ndiye mwanamke wa kwanza katika kipindi cha karne moja katika historia ya Marekani picha yakwe kuwekwa kwenye dola.
Picha hiyo itabadilishwa na ile ya awali ya rais wa saba wa Marekani Andrew Jackson ambaye alikuwa akimiliki watumwa enzi hizo.
Sasa picha ya Andrew Jackson itakuwa nyuma ya noti hiyo.
Noti hiyo itaanza kutumika mwaka 2020 lakini idara ya fedha nchini Marekani imesema ni mwanzo wa kuwakumbuka na kuwaenzi waliopigania haki za kibinadamu nchini humo.
Bi Tubman alizaliwa miaka ya 1800 utumwani jimbo la Maryland. Alifariki 10 Machi, 1913 akiwa eneo la Auburn, jimbo la New York.
Share on Google Plus

. Mtani

Mshana is Tanzanian blogger who writes different news without bias, He provides social, political and sports as well as Entertainment news happening in all parts around the World."STAY ME ALL THE TIME FOR INSTANT UPDATES.."
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment