mtoto mwenye umri wa mwaka mmoja na nusu amepatikana akiwa hai
kwenye vifusi vya jengo lililoporomoka siku ya Ijumaa jijini Nairobi
nchini Kenya.
Jengo hilo la ghorofa sita liliporomoka katika mtaa wa Huruma baada ya mvua kubwa kunyesha.
Akizungumzia hali ya afya ya mtoto huyo, Kamanda wa kitengo cha taifa
cha kudhibiti majanga Pius Maasai amesema kuwa hali ya mtoto huyo
inaendelea kuimalika tangu alipofikishwa hospitalini jana.Kwa mujibu wa gazeti la Daily Nation, msichana huyo alitolewa kwenye vifusi mwendo wa saa kumi usiku na kukimbizwa hospitalini.
Watu 22 wamethibitishwa kufariki na wengine karibu 90 hawajulikani walipo.
- Blogger Comment
- Facebook Comment
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)
0 comments:
Post a Comment