mwanazuoni

Korea Kaskazini: Hotuba ya Trump ni sawa na mbwa anayebweka

Mwanadiplomasia wa cheo cha juu wa Korea Kaskazini ameifananisha hotuba ya Trump kwa Umoja wa Mataia na kibweko cha mbwa.
Akihutubia baraza kuu la Umoja wa Mataifa siku ya Jumatano, Bw Trumo alisema kuwa ataiharibu Korea Kaskazini ikiwa itakuwa tisho kwa Marekani na washirika wake.
Matamshi ya waziri wa mashauri ya nchi za kigeni Ri Yong-ho, ndiyo ya kwanza rasmi ya Korea Kaskazini tangu hotuba ya Trump.




Korea Kaskazini imendelea na mpango wake wa nyuklia na kukiuka maazimio ya Umoja wa Mataifa.
"Ikiwa Bw Trump anafikiri kuwa atatuletea hofu kwa sauti ya mbwa anayebweka basi hiyo kwake ni ndoto."
Akizungumza kuhusu kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jon-un, Bw Trump aliuambia Umoja wa mataifa kuwa Bwana Kim ako katika mikakati ya kujitia kitanzi.
Wanajeshi wa Marekani walio Korea Kusini
Bwana Ri anatarajiwa kutoa hotuba yake kwa Umoja wa Mataifa siku ya Ijumaa.
Wataalamu wanasema kuwa Korea Kaskazni imaharakisha mipango yake ya kuunda makombora ya masafa marefu na mipango yote ya nyuklia.
Tarehe tatu Septemba Korea Kaskazini ilitangaza kuwa imefanya jaribio lake la sita la nyuklia.BBC



Share on Google Plus

. Mtani

Mshana is Tanzanian blogger who writes different news without bias, He provides social, political and sports as well as Entertainment news happening in all parts around the World."STAY ME ALL THE TIME FOR INSTANT UPDATES.."
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment