mwanazuoni

Utafiti: Mbwa mwitu hufanya uamuzi kwa kupiga chafya

Mbwa mwitu hufanya maamuzi yao kwa kupiga kura kupitia kupiga chafya kwa mujibu wa utafiti mpya.
Utafiti huo wa pamoja uliofanywa na wasomi kutoka Swansea, Australia na Marekani ulifuatilia mbwa mwitu walio kwenye hatari ya kuangamia nchini Botswana.
Waligundua kuwa mbwa walitumia chafya kuamua wakati wanaelekea kuwinda baada ya kufanya mikutano inayofahamika kuwa mikutano wa kijamii.
Awali ilikuwa ikifikiriwa kuwa mbwa hao ambayo ni familia ya wanyama walio kwenye hatari zaidi ya kuangamia duniani, walikuwa wakipiga chafya ya kawaida.
Lakini wakati watafiti walirekodi mikutano 68 ya mwa mwitu waligundua kuwa wakati walipiga chafya zaidi walikuwa wakiondoka na kuanza wa kuwinda.
Dr King anasema kuwa chafya hiyo ni lazima ifike kiwango fulani kabla ya wao kuamua kufanya kitu.
Pia uutafiti huo uligundua baadhi ya chafya huwa na uzito kuliko zingine.
Chanzo:bbc
Share on Google Plus

. Mtani

Mshana is Tanzanian blogger who writes different news without bias, He provides social, political and sports as well as Entertainment news happening in all parts around the World."STAY ME ALL THE TIME FOR INSTANT UPDATES.."
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment