mwanazuoni

Mchungaji Peter Msingwa atoa ya moyoni kuhusu Zitto

 Mhe Mbunge Peter Msingwa wa kwanza kulia

Kutokana na sakata linaondelea ndani ya chama cha demokrasia na maendeleo kwa kifupi CHADEMA. Mbunge wa Iringa kupitia chama hicho mhe Peter Msingwa amefunguka yake ya moyoni kuhusu aliyekuwa Naibu katibu mkuu wa chama hicho Mhe Zitto Zuberi Kabwe. Baadhi ya maneno aliyosema bunge huyo ni kama ifuatavyo:


1. ‘Kimsingi nimeonyesha msimamo kwamba nampinga kwa sababu hatendei haki
 chama na ndio msimamo wa kamati kuu, tunachoamini ni kwamba tunatakiwa kupigana wote… kwenye matukio yote muhimu yenye maana ambayo ni ya kukijenga chama hatujashirikiana nae, hatujalia pamoja hatujafurahi pamoja, wenzake tulifurahi pamoja Tarime hakuwepo, tumelia pamoja Arusha wenzake wote mara mbili, Iringa, Morogoro hajakuwepo’

2. ‘Bungeni tumedharauliwa tumetukanwa kwenye matukio yote haya ya msingi hajakuwepo lakini kibaya zaidi amekuja na Waraka huu ambao amefanya na mwenzake Kitila, Waraka wa kukigawa chama kwa hiyo mambo kama haya ndio nimeamua kuonyesha msimamo wangu hadharani na naamini Wabunge wengine ambao tuko nao wataendelea kujitokeza siku zinazokuja kwamba hatuko nae kwenye swala hili hata yeye mwenyewe nimeshaongea nae uso kwa uso, sijali nani ni nani… i don’t care’

3. ‘Mimi ni bora nichukiwe katika uhalisia, sitaki kupendwa kinafiki kama mtu ananichukia ni sawa lakini msimamo wangu ndio huo na kwamba Zitto Kabwe hastahili kuwa Naibu Katibu mkuu wa chama chetu’
Share on Google Plus

. Mtani

Mshana is Tanzanian blogger who writes different news without bias, He provides social, political and sports as well as Entertainment news happening in all parts around the World."STAY ME ALL THE TIME FOR INSTANT UPDATES.."
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment