mwanazuoni

MAREKANI KUWAKUTANISHA ZITTO KABWE NA MAALIM SEIF NOVEMBER 8, 2016


ZITTO Kabwe na Maalim Seif Sharif Hamad kwa pamoja wameitwa jijini Philadelphia, Marekani.

Maalim Seif ni Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF) ambapo Zitto ni Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo.

Wanasiasa hao wameitwa kuhudhuria mkutano mkuu wa Chama cha Demokratiki utakaomthibitisha Hillary Clinton kuwa mgombea urais wa Marekani kupitia chama hicho.

Marekani inatarajia kufanya Uchaguzi Mkuu tarehe 8 Novemba mwaka huu ambapo Clinton atathibitishwa kwenye mkutano huo kupambana na Donald Trump wa Chama cha Republican.

Maalim Seif na Zitto ndio wanasiasa pekee nchini waliopata mwaliko wa kuhudhuria mkutano huo.

Abdallah Khamis, Ofisa Habari wa ACT- Wazalendo amesema wakati Zitto akiwa kwenye mkutano huo, atapata fursa ya kufanya mazungumzo na viongozi mbalimbali wa kisiasa duniani.

Taarifa zinaeleza kuwa, viongozi hao ni wawakilishi wa wanasiasa mahiri kutoka upinzani nchini Tanzania.
Share on Google Plus

. Mtani

Mshana is Tanzanian blogger who writes different news without bias, He provides social, political and sports as well as Entertainment news happening in all parts around the World."STAY ME ALL THE TIME FOR INSTANT UPDATES.."
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment