mwanazuoni

Liverpool 0-0 Manchester United

Mchezo wa kusisimua wa ligi kuu ya soka England umemalizika kwa suluhu ya bila kufungana.
Katika mchezo huo kipindi cha kwanza timu zote zilishambuliana kwa zamu huku kipindi cha pili Liverpool ikishambulia zaidi lango la United.
Kocha wa Liverpool Jurgen Klopp amesema kuwa hakukasirika lakini pia hakufurahishwa na kiwango cha uchezaji wa timu yake.
Klopp pia ameisifu safu ya ulinzi ya Man U na kusema ilikuwa vigumu kushinda kutokana na ulinzi ulivyokuwa imara.
Philippe Coutinho akiachia mkwaju mbele ya wachezaji wa Man u
Image captionPhilippe Coutinho akiachia mkwaju mbele ya wachezaji wa Man u
Kwa upande wake meneja wa Man U Jose Mourinho amesema licha ya kutopata matokeo aliyoyataka lakini ameridhishwa na matokeo hayo.
Amesema si matokeo mabaya kwani waliweza kumzuia hasimu wao wa jadi kuondoka na alama tatu nyumbani kwake.
Katika mchezo huo Ander Herrera aliibuka kuwa mchezaji bora huku akiwa mchezaji aliyegusa mpira mara nyingi kuliko mchezaji yoyote , aligusa mpira mara tisini
Share on Google Plus

. Mtani

Mshana is Tanzanian blogger who writes different news without bias, He provides social, political and sports as well as Entertainment news happening in all parts around the World."STAY ME ALL THE TIME FOR INSTANT UPDATES.."
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment