mwanazuoni

Majaji wawili wa Mahakama Kuu waacha kazi Tanzania

Majaji wawili wa Mahakama Kuu nchini Tanzania wameacha kazi, kwa mujibu wa taarifa kutoka ikulu.
Taarifa hiyo inasema majaji Aloysius Kibuuka Mujulizi na Upendo Hillary Msuya wamewasilisha maombi ya kuacha kazi kwa rais, ambayo yamekubaliwa.
Jaji Mujulizi alikuwa pia mwenyekiti wa tume ya kurekebisha sheria Tanzania.
Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Saidi Meck Sadiki pia ameacha kazi.
Taarifa ya ikulu haijaeleza sababu iliyowafanya maafisa hao watatu kuamua kuomba kuacha kazi.
Share on Google Plus

. Mtani

Mshana is Tanzanian blogger who writes different news without bias, He provides social, political and sports as well as Entertainment news happening in all parts around the World."STAY ME ALL THE TIME FOR INSTANT UPDATES.."
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment