mwanazuoni

Mtoto wa miaka 8 aendesha gari kununua chakula duka la McDonald's

Mtoto mmoja mvulana mwenye umri wa miaka minane katika jimbo la Ohio, aliendesha gari akiwa na dadake mdogo hadi duka la McDolad's baada ya kujifunza kuendesha gari kupitia mtandao wa YouTube.
Jarida na Morning Journal la Ohio lilisema kuwa polisi walipigiwa simu kutoka kwa wenyeji kuhusu mtoto ambaye alikuwa akindesha gari mjini.
Wafanyakazi katika mkahawa wa McDolad's walidhani kuwa ulikuwa ni mchezo wa kuigiza wakati mtoto huyo alisimamisha gari kwenye dirisha kununua chakula.
Mtoto huyo alifuata shera zote za barabara, mtu mmoja aliyeshuhudia alisema.
"Hakugonga chochote njiani, polisi Jacob Koeher kutoka kijiji cha East Palestine alisema.
Mtoto huyo aliwaambia polisi kuwa alijifuza kuendesha gari kwa kutazama video kwenye mtandao wa YouTube.
Inaripotiwa kuwa wazazi wa watoto walikuwa nyumbani wamelala wakati watoto hao waliamua kuchukua funguo za gari.
Baadaye wazazi wao waliitwa kuwachukua na hakuna mashtaka yaliyofunguliwa.
Share on Google Plus

. Mtani

Mshana is Tanzanian blogger who writes different news without bias, He provides social, political and sports as well as Entertainment news happening in all parts around the World."STAY ME ALL THE TIME FOR INSTANT UPDATES.."
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment