mwanazuoni

Trump atangaza kuongeza vikwazo zaidi kwa Korea Kaskazini

Rais Donald Trump amesaini sheria mpya ya kuongeza vikwazo dhidi ya Korea Kaskazini juu ya mpango wake wa nuklia.
Waziri wa fedha wa Marekani ameidhinisha vikwazo hivyo dhidi ya makampuni ya fedha yanayofanya biashara zake ndani ya Korea Kaskazini.
Rais Trump pia amesema kuwa Benki Kuu ya Uchina iliagiza benki nyingine za Uchina kuacha kufanya biashara na Korea Kaskazini.
Hatua hii inakuja katika kipindi cha chini ya wiki mbili baada ya Umoja wa Mataifa kuidhinisha vikwazo ipya dhidi ya taifa hilo kwasdababu ya jaribilo lake la hivi karibuni la nuklia.
Hali ya wasi wasi imetanda katika kipindi cha wiki za hivi karibuni kutokana na hatua ya Korea Kaskazini kufanya majaribio ya makombora ya masafa marefu, licha ya shinikizo kutoka kwa mataifa tajiri zaidi duniani. bbc
Share on Google Plus

. Mtani

Mshana is Tanzanian blogger who writes different news without bias, He provides social, political and sports as well as Entertainment news happening in all parts around the World."STAY ME ALL THE TIME FOR INSTANT UPDATES.."
    Blogger Comment
    Facebook Comment

0 comments:

Post a Comment